Pages

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, April 28, 2012

Drake aanguka tena jukwaani








BIRMINGHAM, Uingereza NI kichekesho. Rapa Drake aliwashangaza mashabiki wake pale alipoanguka wakati akitumbuiza jukwaani huko Uingereza.

Kilichowachekesha mashabiki siyo kuanguka kwake, bali ni ujumbe aliokuwa akiutoa na kitendo hicho.

Inadaiwa rapa huyo alianguka wakati akiimba wimbo Take Care ambao tafsiri yake ni 'Kuwa mwangalifu'.

Kingine kilichowachekesha mashabiki ni kitendo cha rapa huyo kujifanya kama vile alipanga kuanguka na kujikusanya kistaili wakati wa kuinuka.

Walioharibu picha nzima ni mabaunsa ambao baada ya Drake kuanguka na wao kuona hawamuelewi elewi, walimfuata kumuangalia kama yuko sawa, naye alijikausha na kuendelea na onyesho.

Drake aliwahi kuanguka katika shoo mwaka 2009 wakati akiimba wimbo Best I Ever Had na kujitonesha goti lililokuwa likimsumbua

Wastara awaonya wanaomchukulia mumewe!

 

 
 
Kufuati uvumi uliozagaa katika Jiji la Dar ukidai kwamba, msanii anayefanya vizuri kwenye gemu la sinema Bongo, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ amefariki dunia, mkewe Wastara Juma ameibuka akiwataka wazushi hao kuacha mara moja tabia hiyo.

Uvumi huo ulizagaa kuanzia Jumamosi iliyopita huku watu kadhaa wakiandika kwenye kurasa zao za mtandao wa kijamii wa Facebook kuwa, staa huyo ameaga dunia.

Wastara mwenyewe alikiri kupokea simu nyingi kutoka ndani na nje ya nchi zikimpa pole kufuatia ‘kifo’ cha mumewe jambo ambalo alisema linamuumiza sana.

Aidha, Wastara alisema: “Sijui ni binadamu gani aliyeanza kusambaza uzushi huo, lakini nawaomba watu wanaotumia mitandao ya kijamii au kutumia ujumbe mfupi wa maneno kwa simu (sms) kuwa waache upuuzi mara moja".

Na,Darhotwire

Afande Sele atoa somo la Siku ya Kufa

MFALME wa Rhymes kutoka mji kasoro bahari, Morogoro, Afande Sele, amewatahadharisha wasanii wenzake kuwa makini na maisha akiwaambia kuna siku ya kufa kama ilivyo ile ya kuzaliwa.

Afande Sele ambaye alisherehekea siku yake ya kuzaliwa Aprili 24 mwaka huu, amewataka wasanii na Watanzania kwa ujumla kuishi maisha ya amani na upendo.

"Tuna wajibu wa kukumbuka kuwa kama kuna kuzaliwa basi kuna kufa vilevile. Siku ya kuzaliwa itumike kama changamoto kwetu tukitafakari kwanini tupo duniani na makusudi na Mungu kutuumba wanadamu na si wanyama au ndege," alisema.

Afande Sele anakumbukwa sana kwa albamu nne alizowahi kutoa tangu alipojiingiza katika sanaa ya muziki miaka ya tisini.

Albamu hizo ambazo ziliweza kuwashika watu kwa vipindi tofauti ni Mkuki Moyoni, Darubini Kali, Nafsi ya Mtu na Heshima.


Na mwanasporti.

Kidumu jukwaa moja na Msechu

MSANII kutoka nchini Burundi aliyefanikiwa kutamba Afrika Mashariki kutokana na nyimbo zake, Kidumu, anatarajia kufanya shoo akiwa pamoja na Peter Msechu kutoka Tanzania.

Shoo hiyo iliyopangwa kufanyika sehemu maarufu ya kiburudani iliyopo jijini Dar es Salaam ijulikanayo kama Mbalamwezi Beach, inatarajia kufanyika Ijumaa ya Mei 4 mwaka huu.

Kidumu ambaye alikuwa kioo kwa msanii Peter Msechu wakati wa shindano la Tusker Project Fame, atasindikizwa na msanii huyo katika nyimbo zake atakazoziimba usiku huo.

Na mwanasporti.

Dully Sykes aifunua BBM

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Dully Sykes Mr Misifa, ameamua kuingilia kati tabia ya vijana wengi kujikita katika mapenzi ya kwenye mtandao ambayo kwa mujibu wa msanii huyo ni ya kudanganyana.

Dully ambaye hivi sasa ameibuka na wimbo wake mpya 'Mapenzi ya BBM', amesema alisukumwa kuandika mashairi ya wimbo huo kutokana na tabia ya akinadada wengi siku hizo kuutumia mtandao huo kuharakisha ngono kabla ya ndoa.

"Mapenzi ya BBM ni wimbo maalum kwa watu wanaotumia BBM (Blackberry Messenger) tu," alisema.

"Siyo Watanzania wote, lakini wapo wachache wanaoufahamu mtandao huu. Nimeamua kuutoa wimbo huu kutokana na huduma hii ya Blackberry Messenger kushika chati hapa Bongo.

"Yaani mtandao huu umewashawishi akinadada wengi kujiingiza katika masuala ya ngono za mapema ili waweze kupata fedha za kununua simu aina ya Blackberry ili waweze kujiunga katika mtandao huo."


Na, mwanasporti

Barnabas: Magubegube una ujumbe mzito


MSANII aliyesheheni vipaji lukuki kutoka Tanzania, Barnaba Elias Barnabas, amesema kuwa ujumbe uliomo katika wimbo wake wa Magubegube, ni mzito zaidi ya jina la wimbo wenyewe.

"Magubegube ni wimbo ambao nilipanga kuwapa ujumbe wanafunzi wa shule hasa wa kike," anasema Barnabas.

"Kuna wanafunzi ambao wanakwezwa na walimu wao baada ya kuwaridhisha kimapenzi, pia wapo ambao wanafelishwa makusudi hasa wanapokataa kuwaridhisha kimapenzi baadhi ya walimu wenye tabia mbovu.


"Lakini pia ujumbe huo unawaendea na wale wanaopenda ovyo na wenye tabia chafu za kutembea na wake za watu.

"Nilikuwa na mengi na mengine nilishindwa kueleza ndani ya wimbo huo, lakini nina imani umeelimisha vile ipasavyo."


Mwaka huu mwanamuziki huyo alibahatika kupata tuzo ya KTMA baada ya kushirikishwa katika tuzo hizo kwa miaka mitatu mfululizo.

KITABU: Chuo Kikuu cha Hiphop!

 

 
 
Hiki ni kitabu kuhusu Hip Hop kimeandikwa na M.S. HANZI "MALLE" ni denti wa Chuo Cha Ustawi wa jamii Dar es salaam.

Dhumuni la kuandika kitabu hiki ni kutoa mwanga kwa jamii kuhusu Hip Hop na ukweli uliopo kuondoa mtazamo hasi kwamba Hip Hop ni uhuni, ni ya rika fulani tu, kutokana na makosa maarifa utamaduni wa Hip Hop, vijana wengi duniani wanakosea kwa kufikiri vitu/ vitendo kama kuvuta bangi, kunywa vileo, kuvaa mavazi ya wabunifu, kujibandika plasta zenye alama za x, kubeba bastola (gun) au kwenda kujirusha club ndo "Hip Hop" .

Hip Hop inafanywa kimakosa sana na wasanii wengi ambao wanafanya kazi katika nguzo ya ughanaji (uchenguaji). 

Na haya makosa yote kwa kawaida huhamasishwa na kupewa promo na kiwanda cha muziki na washirika wengine ambao hudumaza utamaduni huu kwa kuteka ufahamu wa vijana na maadili yao. 
Kupata kitabu hiki piga simu 0715 076 444 upate copy yako ili uweze kusoma mambo kibao kuhusu Hip Hop.

Na, Darhotwire

Friday, April 27, 2012

ROMA MKATOLIKI KUYAWEKA MAISHA YAKE YA MZIKI KWENYE DOCUMENTARY YAKE MPYA.

 

Msanii anayeiwakilisha TANGA katika bongo fleva ROMA, baada ya kuchukua tuzo mbili za Kilimanjaro kama Msanii bora wa Hip Hop na wimbo wake Mathematics kuchukua kama wimbo bora wa Hip Hip hivi sasa anatengeneza Documentary yake inayoeleza maisha yake kimuziki toka alivyoanza mziki shida alizopitia mpaka kufikia hivi sasa alipofikia.  

Roma akiwa katika studio ya Tongwe Rec akiitengeneza DVD hiyo ambayo amesema nimapema sana kusema itatoka lini ila haitochelewa kutoka na anaamini watu wataipenda na italeta utofauti kidogo maana story iliyomo ndani ya Documentary hiyo iko kitofauti na itamgusa kila mmoja
 
na;Dj Choka

KOFFI CHARLES OLOMIDE AJIPANGA KUGOMBEA UBUNGE KONGO






Koffi Charles Olomide ambaye hivi karibuni amesaini mkataba mwingine na Bia ya SKOL wa kumdhamini kwa miaka miwili ambapo kampuni hiyo itagharaia show zake na kuwalipa mishahara wanamuziki wake.Koffi kwa sasa amezidisa show zake za barani Afrika na kuimarisha zile za Kongo Kinshasa ikiwa ni matokeo ya wanaharakati wa Congo wanaojulikana kama Banakongo au Lecombatant ambao wameongoza kufanya fujo kwenye show za wanamuziki wote ambao walikuwa wakimsupport Rais Kabila kwenye kampeni ambapo Koffi alitunga wimbo kwa ajili ya kuhamasisha wananchi wa Congo kumchagua Kabila ambaye alishinda uchaguzi huo...

Koffi ambaye amesemwa anataka kugombea uchaguzi ujao kwa nafasi ya Ubunge ingawa mwenyewe aliwahi kukanusha hilo lakini watu waliokaribu naye wanasema anampango huo. Hata hivyo wachunguzi wengine wanasema haitakuwa rahisi kwa Koffi kugombea kwa vile si raia wa Kongo akisemwa kuwa anatokea Gabone na wakati mwingine inasemwa anatokea Congo Brazaville na mmoja wa wazazi wake ndio Mkinshasa.

Saturday, April 21, 2012

KURASA ZA MTANDAO WAKIJAMII FB J'MOSI

 
  • Wapendwa....Je ni halali kwa huyu mbunge wetu Halima Mdee kuchangisha pesa kwaajili ya kumsaidia 'LULU na familia yake?Je ni watu wangapi wapo gerezani kwa kuonewa na wengine wana hali duni katika jamii zetu lakini hawana misaada?LULU ni kama nan?kwanini asiiache Sheria ikachukua mkondo wake?
    · · · 17 minutes ago via mobile ·
    • 4 people like this.
      • Rogers Lugalambi uko sawa kabisa
        15 minutes ago · · 1
      • Linus Francis ajui analo fanya kwanini asiwasaidie watoto yatima
        14 minutes ago · · 1
      • James Mortic Hawa wana lao jambo 2,hamna lolote uckute ni ndugu yake.
        13 minutes ago · · 1
      • Neuro Magret Nimeshangazwa sana na hii hali kwa kweli.nimeona angalau niandike,nanyi mchangie mawazo yenu
        13 minutes ago ·
      • Fredy Mhayaya C oni kama kuna kibaya anachotaka kufanya coz inaonekana kama Jamii imemsusa huyu kwann? Yeye asimsadie acha atoe msaada hata wa kisheria coz still now huyu hakuna ushahid wa kwamba alìhusika na kifo cha Kanumba!
        13 minutes ago ·
      • Deogratius George Chambo Atakuwa anamtongozea kaka yake huyo! Babu seya amekaa miaka mingapi jela kwa kuonewa? Kwann wacmchangie kama wana huruma? Nasema ni ushenzi mtupuuuu!
        12 minutes ago · · 1
      • Man Ochu Master It means kuwa haki ya m2 haipatikani bila ya pesa? Au ndo 2amin kuwa pexa ipo juu ya sheria? Vilevile anamaanisha kuwa waliojela wote ni maskini? In general mdee kachemkaa'
        11 minutes ago ·
      • Neuro Magret ¡fredy swali ni kwamba,mbona wengne wapo magerezani kwa kesi za kusingiziwa lakn hakuwasaidia?Lulu ni mtuhumiwa km wengne tu
        11 minutes ago ·
      • Sitty Magomba ANAZINGUA HUYU MDEE
         

kurasa za facebook j'mos

  • MAISA YAMEBADIRIKA XANA
    UKIENDA KUMSARIMIA BA MDOGO WAKO,SHANGAZ YAKO AU KAKA AKO
    WANAONA UMEWAONGEZEA MZIGO
    WANAANZA KUKUULIZA MASWALI MENGI MENGI
    UNAKAA CKU NGAPI
    KWANINI UMEKUJA
    MPAKA UTAGUNDUA WANANIA YA KUKUFUKUZA
     

  • NI KWA UPANDE WA KURASA ZA FACEBOOK ZILIVYO ANDIKWA LEO J'MOSI

    Labels