Pages

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Friday, February 28, 2014

Ostaz Juma: Wasanii na Watangazaji wa redio njaa sana, mtakufa, pesa zangu zinawafanya mnitetemekee



Hiki ndicho alichokiandika kwenye Facebook:

Naona watu mmeguswa sana mimi kuanika Picha za PNC katika mitandao et, tatizo wasanii wa tanzania mnanjaa sana kuanzia watangazaji Radio na wasanii njaa ndio zinazo wasumbua.

Hata mkisema napata pesa kwa utapeli mitandaoni sawa ila ndio pesa zangu na ndio zinawafanya mnitetemekee na kunitaja kwenye vinyimbo vyenu visivyokua na ubora. 


Sawa mimi tapeli naibia watu hilo sikatai nakubali mimi tapeli ila imekuaje msanii wenu kaja kunipigia magoti?

Wasanii wa bongo njaa sana na mtakufa na njaa zenu. Acheni muendelee kunyonywa kwa ujinga wenu shule mmezikimbia tatizo. 

Mnaniona mimi mbaya kuweka picha Za PNC zimewauma sana eeh. Hahahahahahahahahah pesa inaongea hata mseme nini. 

Naomba nyie mabloger na watangazaj msio kua na taaluma wekeni na hii.

Credit:-Bongo5

Monday, February 24, 2014

NEW SONG | KOBA F| DULLY - KIZUNGUMKUTI

NEW SONG | MEDA CLASSIC - I LOVE U

Meneja wa Tip Top Connection Babu Tale amesema kuna uwezekano wa kuja kufanya kazi tena na MB Dogg

Meneja wa Tip Top Connection Babu Tale amesema kuna uwezekano wa kuja kufanya kazi tena na msanii aliyewahi kuwa chini ya kampuni yake kipindi cha nyuma MB Dogg, lakini sasa itakuwa ni kibiashara zaidi tofauti na zamani walipokuwa wanafanya kazi kindugu.

MBDogg
MB Dogg

Akizungumza na Millardayo.com Tale amesema, wapo wasanii kadhaa ambao walitoka Tip Top wanaotaka kufanya naye kazi akiwemo Keisha na Spack, lakini yeye anampango wa kufanya kazi na MB Dogg ambaye pia ametoa wimbo mpya wiki iliyopita uitwao ‘Umenuna’.

“lakini kwa sasa nataka tumuangalie Mb Dogg kwa macho mawili” Alisema Tale. “Mb dogg ana kipaji watu wanaujua uwezo wa Mb Dogg, Mb Dogg sio kama amepotea hapana ila hana uongozi anahitaji promo ya nguvu tu
Babu Tale
akipata hiyo anarudi kupiga hela kama zamani”.
Babu Tale

Akifafanua utaratibu wake wa sasa wa kufanya kazi na wasanii, Tale ambaye ndiye meneja wa Diamond Platnumz kwa sasa, amesema zamani alikuwa akiishi nao kama ndugu lakini sasa hivi anaagalia biashara zaidi.

“Kwa sasa mimi ni mfanyabiashara tofauti na zamani nilipokuwa naishi na wasanii tulikuwa tunaishi kama kaka kwamba matatizo yapo kila mmoja ana matatizo yake mimi nina matatazo na wasanii nao wana matatzio hizo ni sehemu za maisha”.

Tale aliongeza, “wasanii wengi wanaokuja kwangu wanasema wanataka tufanye biashara na
mimi ni mfanyabiashara kama wao, tunabaki kwenye biashara kwa sababu kama naweza kumsimamia msanii ambaye sijatoka nae toka mwanzo kwanini yule niliekuwa nae mwanzo nishindwe kumsimamia na akaleta heshima nchini
akapata mkate wake wa kila siku na mimi nikapata hela”.

Source: Millardayo.com

BARAKA DA PRINCE MSANII MPYA 2014 KUTOKA TETEMESHA ENTERTAINMENT......STAY TUNE


Mambo vipi,

Nachukua fursa hii kumtambulisha msanii mpya wa Tetemesha Records. Anaitwa BARAKA da PRINCE kutoka Mwanza, lakini kwa sasa makazi yake ni Dar ambapo atakuwa hapa moja kwa moja kama makazi yake ya kudumu kikazi.

Amekua chini ya Tetemesha toka mwaka jana lakini kwa kawaida kabla ya kumtoa hadharani msanii mpya hua kuna utaratibu wa ndani katika hatua za kumuandaa ndio sababu ninamtambulisha sasa.

Tegemeeni Video na Audio muda si mrefu kutoka sasa, Video imefanywa na Nisher. Itatangulia kutoka video kisha baada ya wiki itafuata Audio.


Mawasilano ya Barakah:

Simu: 0714 321086

Insta:  @barakah_daprince
Twitter: @barakahdaprince

FB: Barakah da Prince

Best Regards
Kidboy

PROFESSOR JAY NA MRISHO MPOTO WAMEPATA SHAVU LA UBALOZI WA KAMPENI YA KILIMO

Professor Jay ameiambia Bongo5 kuwa wamesaini mkataba wa mfupi na tayari wameshaanza majukumu ya kazi ya kuhamasisha vijana kufanya kilimo mkoani Iringa.
 Mrisho Mpoto akiwa na Professor Jay Iringi
“Watu waliotuteua wanaitwa Ansaf lakini wawakilishi wa serikali ya United States of America ambayo inaitwa ‘One’ kwahiyo hapo kuna Ansaf na One ndio wanetuteua sisi kuwa mabalozi,” amesema Jay.

“Wamesema tuanze kuifanya kwasababu inatakiwa ifanyike kwa wakati huu na hatujasaini mkataba mrefu, tumesaini mkataba tu wa kuwaambia kazi zao walizotaka tufanye Iringa, tumeenda na kuzifanya kwa utiifu kabisa, kwa uaminifu kabisa na kwa uaminifu kabisa na tumewajulisha watu wetu waweze kufanya lakini wametuambia tunaweza kufanya vitu kwa mkataba muda mrefu kidogo.”

Tuesday, February 04, 2014

WAKAZI - CONTROLVERSE (NEW VIDEO & AUDIO)

Huu ni ujio mpya wa Wakazi kabla ya kuachia rasmi albamu yake ya Abacus EP.

Katika ngoma hii amewagusia watu kadhaa hasa wana hiphop lakini ndani ya mashahiri yake anazuia ngoma hiiisichezwe redioni.

“This is just another freestyle song by Wakazi released as a teaser before the release of his abacus EP and his brand new singles also slated for end of the month release. 

In here Wakazi is trading bars & punchlines which seem to be warning shots to fellow emcees who thought he was done and had sold out.” – Wakazi.

SIKU YA SARATANI DUNIANI LEO FEB 04

Saratani ni moja kati ya magonjwa hatari sana duniani.


Siku ya Saratani duniani, huadhimishwa kila Februari 4 ya kila mwaka…Lengo kuu la maadhimisho ya siku hii ni kutoa elimu zaidi kuhusiana na kujikinga, kwenda kupima na jinsi ya kupata matibabu endapo utagundulika kama umeathirika na Saratani.

Kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huu wa kansa kufikia mwaka 2020 ndiyo lengo kuu la Union For International Cancer Control (UICC), taasisi inayohusika na kuandaa na kuratibu siku hii duniani kwa ujumla.


Mapambano dhidi ya Saratani…Inawezekana endapo watu wote watapewa elimu ya kutosha juu ya dalili nyemelezi ambazo huashiria mwanzo za ugonjwa huu; jinsi ya kujikinga pamoja njia zipi zitumike kumpatia matibabu muathirikia wa saratani.


Taasisi ya saratani ya Ocean Road imesema inakabiliwa na wingi wa wagonjwa wanaofika katika taasisi hiyo ambapo kwa mwaka jana pekee, wagonjwa 5244 wapya walihudumiwa na taasisi hiyo. 

Tanzania ni miongoni mwa nchi katika Jangwa la Sahara, linalokabiliwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa saratani.


Akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Saratani Duniani, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road ,Prof Twalib Ngoma, amesema licha ya ugonjwa huo kuwepo nchini kwa miaka mingi na kusababisha vifo vya watu wengi, bado jamii haina elimu sahihi kuhusiana na ugonjwa huo.

Lakini pia Taasisi hiyo, inakabiliwa na upungufu wa vitendea kazi Takwimu za ugonjwa wa Saratani zinaonyesha kuwa Tanzania kila mwaka wanagundulika wagonjwa wapya 21,180 na zaidi ya watu 16,000 hufarika kila mwaka kutokana na ugonjwa huo wa saratani.

Monday, February 03, 2014

YULE DADA ALIYEMCHUKULIA WEMA SEPETU BWANA , ATIA AIBU BAADA YA PICHA ZAKE ZA UTUPU KUONEKANA MTANDAONI.


Rafiki kipenzi wa Wema Sepetu mwanadada Naima ambaye ndiyo anamiliki mpenzi wa zamani wa shosti yake anayejulikana kwa jina la Clement ambaye ni kigogo na pedeshee wa mjin hapa, hivi karibuni aliachia picha mtandaoni akiwa mtupu na kufanya watu washikwe na mshangao na kumshangaa dada huyu.

Lady Jay Dee kuachia rasmi video ya 'Historia' February 8

Lady Jay Dee kuachia rasmi video ya 'Historia' February 8, mashabiki 20 walio Facebook kuhudhuria party maalum ya kuitambulisha

Mitandao ya kijamii inazidi kuwa njia rahisi na kubwa zaidi kwa wasanii kuwasiliana moja kwa moja na mashabiki wao na hata kufahamu ni kwa jinsi gani wanaelewa na kuwafuatilia kwa karibu, na zaidi kutoa maoni yao moja kwa moja kuhusu kinachofanywa na wasanii hao.
Mwimbaji wa kike wa bongo flava mwenye mafanikio makubwa, Judith Wambura aka Lady Jay Dee amebreak habari njema kwa mashabiki wake wa mitandao ya kijamii ambao wanafikia 225,722 kwa upande wa Facebook na zaidi ya 66, 400 wanaomfuata kwenye Twitter, kuwa ataitoa rasmi video ya wimbo wake wa ‘Historia’, February 8 mwaka huu kupitia party maalum, na watu 20 kati yao watapata nafasi ya kuhudhuria tukio hilo.
Mashabiki wa Facebook wamepewa nafasi zaidi ambapo kigezo ni kujibu maswali yatakayotolewa na mwimbaji huyo wa Joto Hasira.
“Video ya Historia iko tayari na itatoka Jumamosi ya tar 8 february 2014 kwenye party maalum ya kuitambulisha, na kutoka humu facebook nitaalika watu 20 wa kuja kuiangalia kwa mara ya kwanza kabla haijaruka kwenye TV zote.. 
Swali litakuja na 20 wa mwanzo watakaopatia nitajumuika nao. Usicheze mbali.” Ameandika Lady Jay Dee.

Young Dee: Muziki umeirudisha heshima ya familia yangu, nimeikomboa nyumba ya familia kwa kulipa deni, ilikuwa iuzwe million 37

Wakati ambapo rappers wengi wa Tanzania wanalalamika kuwa muziki hauwalipi kivile kutokana na kazi kubwa wanayofanya, kuna baadhi ya rappers ambao wana mtazamo tofauti na kwao rap ya Tanzania imewawezesha kufanya vitu vikubwa kuanzia katika ngazi ya familia, na wanaushukuru muziki wa Tanzania kwa hatua hiyo.
Rapper mwenye uwezo mkubwa wa kurap kwa Kiswahili fasaha, Young Dee, ni mmoja kati ya rappers ambao kwao muziki umewatendea haki na hawaoni haja ya kulalamika.
Akiongea na tovuti ya Times Fm, Young Dee amesema anauheshimu sana muziki wa Tanzania kwa kuwa umeweza kusaidia kuirudisha heshima ya familia yake baada ya kuweza kutumia kipato anachokipata kwenye muziki kuikomboa nyumba ya familia yao iliyotakiwa kuuzwa ili kufidia deni la marehemu baba yake la kiasi cha shilingi million 8, na ilitakiwa kuuzwa shilingi million 37 .
“Marehemu baba yangu alikuwa ana deni kubwa ambalo hakuna mtu ambaye alikuwa anaweza kuilipa hilo, kwa hiyo ilikuwa ni nyumba ambayo iliikuwa imekaa imetelekezwa na imeharibika japo ilikuwa imejengwa kwa mfumo wa kisasa kidogo lakini bado inahitaji kuongezewa nguvu. Young Dee ameiambia tovuti ya Times Fm.
“Kwa hiyo niliweza kutumia pesa yangu kuclear hilo deni na kuweza kuiregister upya kama nyumba yangu sasa. Kwa sababu ilikuwa na madeni na ilikuwa iuzwe kwa thamani ya million 37. Kwa hiyo hilo deni limeweza kuli-clear, kwa hiyo hicho ni kikubwa zaidi kwa hiyo sasa hivi iko pale inanisubiri mimi nikusanye tena nguvu nimalizie mambo machache niweze kuhamia.” Ameongeza.
Amesema kwa kuzingatia hilo, mama yake ameweza kuwa na furaha zaidi na muziki anaoufanya hata kuliko yeye mwenyewe (Young Dee). Ameongeza kuwa kuwa kwa muda mrefu yeye amekuwa akiishi katika nyumba za kupanga lakini kufikia mwezi wa nane atakuwa amemaliza kuikarabati nyumba hiyo na kuhamia.
“Kufikia mwezi wa nane naweza kumpigia simu mama yangu na kumwambia, mama njoo ukae kwangu.”
Kwa upande mwingine, Young Dee amesema video ya Kijukuu ilimlipa zaidi ya gharama alizotumia kuifanya na kwamba ana mpango wa kufanya video nyingine kali ya wimbo wake ‘Fununu’ aliofanya na mwana FA na kwamba ana ma-director wawili kichwani kwake akiwemo Nisher aliyefanya video ya ‘Kijukuu’.

DJ D-Ommy wa Times FM kuachia mixtape maalum kwa wapendanao ‘The Valentine’s Heart Felt Mixtape’

Dj D-Ommy wa Times Fm kuachia mixtape maalum kwa wapendanao

Dj D-Ommy aka The Number One Freestyle Dj in Tanzania, ataachia mixtape yake siku ya wapendao (February 14), mixtape aliyoipa jina la ‘The Valentine’s Heart Felt Mixtape’, maalum kwa ajili ya wapendao.
‘The Valentine’s Heart Felt’ itakuwa mixtape ya tatu kutoka kwenye mikono ya Dj D-Ommy ikizifuatia mixtape zilizopita ambazo ni The Return of the Transform Master na Afro Pop Cutz.

HAJA NDIYO MAJINA YANAYOWANIA ''ACTION & CUT VIEWER'S CHOICE AWARDS 2014'' TANZANIA

Muigizaji wa filamu na mtangazaji wa kipindi cha Action and Cut kinachorushwa na kituo cha runinga cha Channel Ten, Bond Bin Sinan aameandaa tuzo za wasanii wa filamu nchini kupitia jina la kipichi hicho.
film_logo
Tayari majina ya watakaowania tuzo hizo yametoka. 

Jinsi ya kumchagua msanii unayemtaka, tuma jila la msanii kwa kila categories kwenda namba 0782 555 465. 

Zoezi hili ni kwa wiki 7 na baada ya hapo tarehe ya tuzo itatajwa.

Hii ndio orodha nzima.

BEST ACTOR

Jacob Stephen ( SHIKAMOO MZEE)
Mohammed Mwikongi ( WAITING SOUL )
Simon Mwampagata Radio ( MAHABA NIUWE)
Hemed Suleiman ( STELLA )
Steve Mengere Nyerere ( GET OUT )
Salim Mohammed Gabo ( BADO NATAFUTA)

BEST ACTRESS

Rose Ndauka ( WAITING SOUL)
Irene Paul ( LOVE & POWER)
Wastara Juma ( Mr & Mrs SAJUKI)
Irene Uwoya ( QUESTIONS MARC)
Elizabeth Michael Lulu ( FOOLISH AGE)
Jacline Wolper ( MAHABA NIUWE)

BEST UPCOMING MALE

Rammy Valid ( FAN’S DEATH)
Mohammed Mussa ( MBEGU)
Gerry Wa Rhymes ( STELLA)

BEST UPCOMING FEMALE

Wellu Sengu ( MATILDA)
Janeth Lameck ( BIKIRA KIDAWA)
Najma Dattan ( FAN’S DEATH)

BEST DIRECTOR

Vincent Kigosi (TWISTED)
Issa Mussa Cloud (SHAHADA)
John Lister (PUMBA)
Jackson Kabirigi ( NGUVU YA IMANI)
Lamata ( Mr & Mrs SAJUKI)
Kulwa Kikumba Dude ( MELVIN)

BEST FILM

Twisted ( RJ FILM COMPANY)
Nguvu ya Imani ( )
Shikamoo Mzee ( JERUSALEM FILM COMPANY)
Tikisa (NISHA’S FILM COMPANY)
Mr & Mrs Sajuki (WAJEY FILM COMPANY)

BEST D.O.P

Kabuti Onyango (TIKISA)
Farid Uwezo (TWISTED)
Hassan Maimbari (Mr & Mrs SAJUKI)
Rashid Mrutu ( APLE)
Timothy Conrald ( NGUVU YA IMANI)

BEST EDITOR

Farid Uwezo ( TWISTED )
Timmoth Conrald ( NGUVU YA IMANI)
Hassan Maimbari (Mr & Mrs SAJUKI)
Zakayo Magulu ( LOVE & POWER)
Rashid Mrutu (APLE)

BEST COMEDIAN

Amri Athuman King Majuto ( SHIKAMOO MZEE)
Hadji Salem Mboto ( NYOTA YANGU )
Kitale ( MORE THAN A LIAR)
Mahsein Awadh Dr. Chen ( MAJANGA)

BEST COMEDIAN

Amri Athuman King Majuto ( SHIKAMOO MZEE)
Hadji Salem Mboto ( NYOTA YANGU )
Kitale ( MORE THAN A LIAR)
Mahsein Awadh Dr. Chen ( MAJANGA)

BEST ACTION MOVIE

C.I.D
Bongo Mafia
Double J Final
Damu Nzito
Step by Step

CHANZO:-BONGO5.COM

Sunday, February 02, 2014

RAIS KIKWETE AONGOZA MATEMBEZI YA MSHIKAMANO YA MIAKA 37 YA CCM JIJINI MBEYA......KUHUTUBIA TAIFA MCHANA HUU

 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Rais Jakaya Kikwete  akiwapungia mkono baadhi ya Wananchi (hawapo pichani),walioshirikia matembezi ya mshikamano yaliyoanzia viwanja vya SIDO,kuelekea kwenye bustani iliyopo nje ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya mapema leo asubuhi,ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya kusherehekea miaka 37 kuzaliwa kwa chama cha CCM.

Kushoto kati ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Mbozi Mashariki,Mh.Godfrey Zambi,Katibu Mkuu wa chama hicho,ndugu Kinana pamoja na Katibu wa Uchumi na Fedha,Bi Zakia Meghji wakishiriki matembezii hayo yaliyofana kwa kiasi kikubwa jijini humo.

Rais Kikwete ambaye ndiye mgeni rasmi wa sherehe hizo atahutubia leo  mchana kwenye maadhimisho ya sherehe hizo zitakazofanyika katika uwanja wa Sokoine mkoani humo.
Rais Kikwete akiongoza  matembezi ya mshikamano yaliyoanzia viwanja vya SIDO akiwa sambamba na baadhi ya watoto,kuelekea kwenye bustani iliyopo nje ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya,ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya kusherehekea miaka 37 kuzaliwa kwa chama cha CCM.Kushoto kati ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Mbozi Mashariki,Mh.Godfrey Zambi,Katibu Mkuu wa chama hicho,ndugu Kinana pamoja na Katibu wa Uchumi na Fedha,Bi Zakia Meghji wakishiriki matembezii hayo yaliyofana kwa kiasi kikubwa jijini humo. 
 Baadhi ya vijana wakereketwa na chama cha CCM wakiwa na mabango yao. 
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Rais Jakaya Kikwete  (pilia kulia) akiwa tayari kuongoza wanachana na Wananchi (hawapo pichani) kushiriki matembezi ya mshikamano yaliyoanzia viwanja vya SIDO,kuelekea kwenye bustani iliyopo nje ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya mapema leo asubuhi,ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya kusherehekea miaka 37 kuzaliwa kwa chama cha CCM.Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM,Bwa.Phillip Mangula,wa tatu kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Mbozi Mashariki,Mh.Godfrey Zambi,Katibu Mkuu wa chama hicho,ndugu Kinana pamoja na Katibu wa Uchumi na Fedha,Bi Zakia Meghji pamoja na Waziri Ofisi ya Rais asiye na Wizara maalum,Prof Mark Mwandosya wakiwa tayai kuyaanza matembezi hayo.
 Rais Kikwete akizungumza na baadhi ya watoto waliokuwa miongoni mwa watoto waliojitokeza kushiriki  matembezi ya mshikamano yaliyoanzia viwanja vya SIDO mapema leo asubuhi kuelekea kwenye bustani iliyopo nje ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya,ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya kusherehekea miaka 37 kuzaliwa kwa chama cha CCM.
 Baadhi ya Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakishiriki kuchukua matukio yaliyokuwa yakijiri kwenye matembezi ya mshikamano yaliyoanzia viwanja vya SIDO mapema leo asubuhi kuelekea kwenye bustani iliyopo nje ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya,ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya kusherehekea miaka 37 kuzaliwa kwa chama cha CCM.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Rais Jakaya Kikwete akipokelewa na viongozi wa chama hicho ngazi za juu,pichani akisalimiana na  Katibu Mkuu wa chama hicho,ndugu Kinana na anaeshuhudia pichani kati ni Makamu Mwenyekiti wa CCM,Mh.Phillip Mangula,tayari kwa kuongoza matembezi ya mshikamano yaliyoanzia viwanja vya SIDO,kuelekea kwenye bustani iliyopo nje ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya,ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya kusherehekea miaka 37 kuzaliwa kwa chama cha CCM. 
 Baadhi ya Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa matembezi ya mshikamano yaliyoanzia viwanja vya SIDO mapema leo asubuhi kuelekea kwenye bustani iliyopo nje ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya,ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya kusherehekea miaka 37 kuzaliwa kwa chama cha CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akifurahi jambo na Waziri Ofisi ya Rais asiye na Wizara maalum,Prof Mark Mwandosya 
 Ndugu Kinana akizunguza jambo na Mwigulu Nchemba kabla ya kuanza matembezi ya mshikamano. 
  Msafara wa Rais ukiwasili sehemu ya kuanza matembezi ya mshikamano. 
 Mambo ya matembezi ya mshikamani yakiwa yameiva
 Rais Kikwete pia aliungana na Watoto katika matembezi hayo. 
 Mwenyekiti wa CCM,Rais Kikwete akiwasili kwenye bustani za uwanja wa Sokoine kufikia kilele cha matembezi ya mshikamano
 Sehemu ya Wananchi na wakereketwa wanachama mbalimbali wa wa CC Mwakiwa wamekusanyika kwa pamoja tayari kumsikiliza Rais Kikwete mara baada ya kumaliza matembezi hayo yalifanikiwa kwa kiasi kikubwa.
 Baada ya kumaliza matembezi ya mshikamano viongozi wa juu wa CCM,wakisiliza utaratibu wa kuadhimisha sherehe za miaka 37 ya kuzaliwa kwa chama hicho.

Rais Kikwete akizungumza machache mara baada ya kumaliza matembezi ya mshikamano,Rais Kikwete atakuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo zitakazoanza mapema leo mchana ndani ya uwanja wa Sokoine,jijin Mbeya.

-EDDY BLOG

02|02|2014 KITULO FM TOP TWENTY

Nafasi wiki hili
Jina la Wimbo & Msanii
Wiki lililopita
20
Wacha Waseme – Ambanto ft Aslay (Ingizo Jipya)
-
19
Kula Gambe – Shilla Vee (Ingizo Jipya)
-
18
Kioo – Jaguar
20 Last week
17
Mimi na wewe – Dayna Nyange
19 Last week
16
Siri ya Mchezo – Fid Q F| Juma Nature
15 Last week
15
The Monster – Eminem F| Rihanna
14 Last week
14
Bound 2 – Rick Ross “Rozay”
18 Last week
13
Roho yangu – Rich Mavoko
13 For 2 weeks
12
Wanitaka – Belle 9
12 For 2 weeks
11
Monifere – Gosby F| Jux & Vanessa Mdee
08 Last week
10
Kajiinamia – Abdu Kiba F| Ali Kiba
11 Last week
09
Come Over – Vanessa Mdee a.k.a Vee Money
07 Last week
08
Nakula Ujana – Ney wamitego
04 Last week
07
Basi njoo kariakoo – Abby Skillz F| Ali kiba & Shetta
06 Last week
06
Mapenzi nguvu ya Dunia – Councilor
10 Last week
05
Mtemi Pesa – Squeeza F| Belle 9
05 For 2 weeks
04
Nothing to Me – P Bling
09 Last week
03
Chapa Nyingine – Chege F| Gift
02 Last week
02
Timber – Pitbull F| Ke$ha
03 Last Week
Bonus Trk
Historia – Lady JayDee
-
01
Chelewa – Navy Kenzo (Aika,NahReal & Weestar)
1 For 3 Weeks

*ORODHA YA NYIMBO 20 IMEANDALIWA NA:-Ergon Elly
*TOP 20 IMESIMAMIWA NA:-Ergon Elly
*MAONI|USHAURI|KURA TUMA KUPITIA:-
(i)Email:-ergonsanga@yahoo.com AU
kitulofm@yahoo.com
(ii)Simu:-+255 718 742 990 AU
+255 759 522533

Jumapili Njema!!!!

@2014

Labels