Pages

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, February 01, 2014

OGOPA DEEJAYS YA KENYA YASITISHA MIKATABA YA WASANII WAKE

Jina la Ogopa Deejays limekuwa zaidi katika miaka ya karibuni nchini Tanzania kutokana na wasanii wengi wa Bongo kufanya video na kampuni hiyo, ambayo ilianzishwa miaka 1990 ikiwa studio ya kurekodi audio pekee
kwa wakati huo.


ogopa3
Kwa mujibu wa mtandao wa GHAFLA, Ogopa deejays imesitisha mikataba ya baadhi ya wasanii ambao ilikuwa ikiwasimamia kwa miaka kadhaa iliyopita.
Avril
Wasanii waliopitiwa na panga hilo ni pamoja na mwimbaji mrembo Avril ambaye taarifa za hivi karibuni zinasema anategemea kuhamishia makazi
yake Afrika Kuisni, yaliko makazi ya mchumba wake wanaetarajia kufunga ndoa hivi karibuni.
marya
Marya
Wasanii wengine ambao mikataba yao imesitishwa na Ogopa ni Marya,
Colonel Moustapha na Kenzo.
Mustafa
Colonel Moustapha

Mmiliki wa studio ya Ogopa Lucas Bikedo, ametoa maelezo kuhusu taarifa zilizoenea za kusitishwa kwa mikataba ya baadhi ya wasanii wake,

“Kila mara mashirika hufanya mapitio ya ndani kutathmini utendaji dhidi ya matarajio. 

Wakati wa mapitio, maamuzi magumu hutakiwa
kufanyika”.

Ilisema taarifa kutoka kwa Lucas baada ya GHAFLA kutaka kupata ufafanuzi.

“Sehemu ya matarajio yetu imekuwa ni kutafuta na kutoa vipaji ambavyo vinaweza kushindana nje ya Afrika Mashariki. 

Katika siku za nyuma mfumo huu umeweza kufanya kazi vizuri sana. 

Hata hivyo, sekta ya burudani imebadilika kwa haraka na uwekezaji uliohusika kuleta mafanikio unakuwa kila siku.

Kama biashara, uwekezaji ni lazima ulete faida ndani ya wakati uliokusudiwa. 

Hii itaruhusu uwekezaji mpya ili uchumi ukue. Na hii inawezekana tu katika mazingira ambapo vipaji vinavyohusika vinapotambua kuwa hata kama kuna kushinda ama kushindwa ni lazima uendele kujitahidi kadri ya uwezo katika kazi iliyo mbele. 

Hakuna mbadala wa kufanya kazi kwa bidii, malengo na nidhamu.

Mtindo wa biashara wa sasa wa kusaini vipaji ni hatari sana na una assumptions nyingi mno.

Sehemu ya tathmini inayoendelea inahusisha na
kuangalia mtindo huu na umuhimu wake katika hali ya sasa.”

Hata hivyo Lucas hakutoa majibu ya moja kwa moja kuhusu wasanii wanaodaiwa kupoteza nafasi zao Ogopa deejays.

*Source: GHALFA*


CINDY SANYU (UGANDA) NA DAYNA NYANGE (TZ) KWENYE STAGE MOJA

MSANII KATY PERRY AANDIKA REKODI KUWA MTU WA KWANZA KUFIKISHA FOLLOWERS MILIONI 50 KATIKA MTANDAO WA KIJAMII WA TWITTER

Katy-Perry-katy-perry-16324222-1920-1080
Katy Perry awa mtu wa kwanza duniani kufikisha followers milioni 50 kwenye Twitter Kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa mtandao wa Twitter, Katy Perry amekuwa mtu wa kwanza duniani kufikisha followers milioni 50. 

Katika nafasi ya pili yupo Justin Bieber akiwa na zaidi ya followers milioni 49. 

Nafasi ya tatu imekamatwa na Rais Barack Obama wa Marekani akiwa na zaidi ya followers milioni 41.

Hata hivyo Katy Perry hatweets sana kama Justin na Obama kwakuwa hadi sasa ameshatweet mara 5370, Bieber mara 25,000 na Obama tweets 11,000.

Katy ametweet: Oh yeah AND we grew to 50 million Katycats! Eh, regular
day at the office.

PRODUCER LAMAR ADAI KUWA NA MPANGO WA KUNUNUA NDEGE BINAFSI

IMG_8021

Kila mmoja ana ndoto zake za kuwa na kitu cha thamani maishani lakini ndoto aliyonayo producer Lamar, kwa wengi inaweza kuonekana kama kubwa mno kwake. 

Lamar ameiambia East Africa Radio kuwa ana mpango wa kununua ndege yake binafsi atakayoitumia kuzunguka popote anapotaka.

Kuonesha kwamba anataka kuanza kuishi ndoto hiyo mapema iwezekanavyo, Lamar ameshaanza kufanya mazungumzo na wauzaji wa ndege hizo ili ajipatie yake mapema.

Lamar si mtu pekee mwenye ndoto ya kumiliki ndege binafsi. 

AY pia ameamua kujifunza urubani kwa kuamini kuwa siku moja anaweza naye anaweza kumiliki yake mwenyewe.

“Wanakuambia dream big, thing big. Fikiria kitu ambacho ni kikubwa zaidi
ya uwezo wako. 

Kwahiyo naweza kusema kuwa kila kitu kinawezekana kwasababu hata wale wenye private jet wakati wakiwa wadogo au wakati hawawezi kuafford walikuwa wanafikiria kuwa kuna siku nao wanaweza kuwa na private jet, so vyote viwili vinawezekana,” AY aliiambia Bongo5.

NEW AUDIO:- D KNOB F| MWASITI - NISHIKE MKONO

D knob

Ni muda mrefu umepita bila kusikia kazi mpya kutoka kwa D-Knob, wala habari zake kutokana na ukimya wake wa muda mrefu, lakini sasa hatimaye rapper huyo wa ‘Elimu ya Mitaani’ anatarajia kuvunja ukimya huo kwa kutoa single mpya aliyomshirikisha Mwasiti.

Single hiyo inayoitwa ‘Nishike Mkono’imefanywa na Producer Villy na inatarajiwa kutoka Jumanne ijayo February 4.

Monday, January 27, 2014

MAREHEMU MZEE DUDE WA FUTUHI KUZIKWALEO JUMANNE HUKO MWANZA

Msanii wa kundi la FUTUHI linalo rusha kazi zake kupitia Star TV, Mzee Dude amefariki dunia leo mida ya saa 11 jioni akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Bugando ya jijini Mwanza ambako alilazwa mara baada ya kuzidiwa ugonjwa wa muda mrefu aliokuwa nao kwa figo kushindwa kufanya kazi.
Enzi za uhai wake Mzee Dude alikuwa mchezhi na mbunifu wa hali ya juu kuwavunja watu mbavu.
Mzee Dude atazikwa kesho jijini Mwanza majira ya alasili na taarifa kamili utazipata hapa.

Mpiga tumba mahiri katika muziki wa dansi hapa nchini SOUD MOHAMED aka MCD amefariki dunia

Mpiga tumba mahiri katika muziki wa dansi hapa nchini SOUD MOHAMED aka MCD amefariki dunia usiku huu katika hospital iliyopo mjini Moshi inayoitwa KCMC mkoa wa Kilimanjaro. 

CIMG2415

Marehemu MCD alikwenda kutibiwa alikuwa akiumwa kwa siku kadhaa ingawa bado hatujapewa taarifa kamili ni kipi kilichokuwa kikimsumbua hadi mauti kumkuta.


Taarifa hizi za kifo cha MCD zimetolewa na msemaji wa bendi Twanga Pepeta Hassan Rehami.


MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU SOUD MOHAMED MAHALI PEMA PEPONI.....Ameen.


SHILOLE aka SHISHI BYBEE tarehe 31.1.14 anakuja na WIMBO MPYA la kufungia mwezi January

IMG-20140127-WA0004

IMG-20140127-WA0003
Mwanadada SHILOLE aka SHISHI BYBEE anatarajia kutoa wimbo wake mpya kabisa kwa mwaka huu 2014 alioupa jina la CHUNA BUZI. 

Shilole ambaye ni mwigizaji wa Bongo Movie na pia ni msanii wa Bongo Fleva amesema kuwa anatarajia mambo makubwa sana kwa mwaka huu 2014 kama mungu atamjalia pumzi.

Shilole ambaye bado anatesa na kichupa chake kinachoitwa NAKOMAA NA JIJI amesema CHUNA BUZI nimwendelezo tu wa nyimbo zake lakini mashabiki wake wanaona kama majina anayoyachagua kukaa kwenye nyimbo zake yanaonekana kama anayaimba maisha yake.

Wimbo huu mpya ameufanyia pale Mazuu Rec chini ya Producer Mazuu.

Chanzo:-Dj Choka Music

RAPPER YOUNG KILLER MSODOKI AMERUDI CLASS

Young Killer Msodoki, rapper mwenye umri mdogo aliyefanikiwa kuiteka Tanzania na hata kuifikisha sauti yake Marekani na kumpata shabiki ‘mzungu’ aliyejirekodi na kuweka ujumbe wake youtube kueleza jinsi anavyomkubali, sasa amefanikiwa kuishi ndoto yake ya kujiendeleza kimasomo.

Rapper huyo ambaye hivi karibuni alieleza wazi kuwa anahitaji msaada wa kifedha ili aweze kurudi shule, ameingia rasmi darasani kusomea Information Technology (IT).

“Am..back…class…”, ameandika Instagram na kupost picha inayomuonesha akiwa anasoma huku ana headphone shingoni (Muziki na Shule).

Young Killer amejiunga na chuo kiitwacho ‘Green Pasture’ wiki mbili zilizopita. Kuanzia katikati ya mwaka jana, Young Killer alianza kuweka wazi wazo lake la kutaka kurudi shule na aliwahi kutaja masomo ya IT kuwa ndiyo ambayo angependa kusomea.

Tunamtakia kila la kheri kwa hatua nzuri aliyoipiga.

WIMBO MPYA | 20% - SUBIRA

Sunday, January 05, 2014

Taarifa kamili kuhusu boti iliyotupa watu 10 baharini ikitokea Pemba.

bahari 
Boti ya Kilimanjaro II ikitokea Pemba kuelekea Unguja imepigwa na dhoruba leo Jan 5 2014 kwenye saa nne asubuhi na kuponea kuzama ilipokua kwenye eneo hatari la Nungwi ambapo ilizama kidogo mbele na kunyanyuka hivyo watu wa mbele wote wakaachwa lakini pamoja na kuwatupa hao watu kwenye maji Nahodha akafanya uamuzi mwingine mgumu.

Aliona akisimama ili kuwaokoa wale watu boti yote ingezama pale hivyo akaamua kuendelea na safari lakini kabla ya kuondoka watu kadhaa ndani ya boti wakajitolea kuwatupia life jacket wale waliotupwa kwenye maji ambapo shuhuda anasema kama mtu hajui kuogelea anaweza kupoteza maisha kwa sababu hawakua wamejiandaa kwenye tukio hili la ghafla na sio wote wamepata vifaa hivyo vya kujiokoa.

Shuhuda mmoja anasema ‘yani boti ilizama ghafla mbele hivyo watu wakatupwa kwenye maji kwenye hii sehemu ambayo kuna mkondo wa maji, upepo ulikua mkali sana yani unaona watu wanajaribu kujiokoa mabegi na vitu vingine vinaonekana juu ya maji’

BREAKING NEWS: BOTI YA MV KILIMANJARO II KUTOKA PEMBA KUELEKEA UNGUJA YANUSURIKA KUZAMA

Habari zilizotufikia hivi punde zinasema boti ya Kilimanjaro 2 iliyokuwa ikitoka Pemba kuelekea Ugunja inasemekana imepingwa na dhoruba kali na kunusurika kuzama, inadaiwa kuna vifo vimetokea. 
 
Ukweli ni kwamba wimbi kubwa liliipiga boat na kusababisha hali ya tafrani. Nimetoka kuongea na mamlaka ya bandari sasa hivi na boat iko njiani inakuja unguja iko maeneo ya Beit ras sasa hivi. Haijazama  na iliondoka na abiria watu wazima 269, watoto 60 na mabaharia 8 wote wako salama.

Wimbi kubwa liliipiga likachukua mabegi na baadhi ya life jackets. Injini za boat zilizima, ilibidi watulie kwa muda kuona kama wimbi lilichukua na baadhi ya abiria lakini hakuna hata mtu mmoja aliyeachwa.
 
Nakumbuka mamlaka ya hali ya hewa walitoa tahadhari kuhusu mchafuko wa bahari hizi siku.

CHANZO:-JAMII FORUM NA CLOUDS FM

ORODHA YA NYIMBO 20 ZA REDIO KITULO FM JUMAPILI 05|01|2014



NAFASI
JINA LA WIMBO & MSANII
20:-
Nothin’ to Me – PBling
19:-
Kajiinamia – Abdu kiba F| Alli kiba
18:-
Mapenzi nguvu ya Dunia – Councillor
17:-
Chapa Nyingine – Chegge F| Gift
16:-
Come Over – Vanessa mdee
15:-
Umependeza – Rachel
14:-
Tema Mate Tuwachape – Madee
13:-
Tebiba Bingi – Irene
12:-
Drive Slow – JCB F| Prof Jay
11:-
Sijiwezi – Maua Sama
10:-
Timber – Pitbull F| Ke$ha
09:-
Siri ya Mchezo – Fid Q F| Juma Nature
08:-
Chelewa – Navy kenzo (aika,NahReal & Weestar)
07:-
Usihukumu – Criss wamarya
06:-
The Monster – Eminem F| Rihanna
05:-
Monifere – Gosby F| Jux & Vanessa Mdee
04:-
Roho yangu – Rich Mavoko
03:-
Basi njoo kariakoo – Abby Skillz  F| Alli kiba & Shetta
02:-
Nakula Ujana – Ney wamitego
Bonus Track
Pendo – Y Tony
01:-
Mtemi Pesa – Squizer F| Belle 9


Wednesday, January 01, 2014

(Official Music Video) Nay wa Mitego – Nakula ujana

MSANII M.I.A HAYUPO TENA ROCK NATION RECORD LEBEL YA JAY Z

Unakumbuka Mstari Wa Jay z "I Dont Get Dropt, I Drop The Lebel" Inaonekana M.I.A kautumia hapa. 
Mwaka 2014 ameanza tofauti kwa lebel ya Rapper Jay Z kwa kupoteza mmoja ya wasanii wakali kwenye himaya yake.

Huyu M.I.A ni msanii mwenye kipaji tofauti na wasanii wengine na kama hufuatili vitu adimu kwenye game basi kazi zake zimekupita. 

M.I.A Alikuwa chini ya usimamizi wa Rock Nation na alikuwa akisimamiwa kama msanii na kazi zake. 
Msanii huyu alitangaza kupitia kurasa yake ya Twitter kuwa " Anaondoka Rock Nation na anatoa shukrani zake kwa wote waliompa nguvu kupitia kazi yake ya MATANGI "
M.I.A Mwenye miaka 38 alianza kufanya kazi na Jay-Z mwezi May mwaka 2012 na kujiunga na wasanii kama Rihanna, J. Cole, Meek Mill na Wale.

HII NI TAARIFA YA IKULU KUHUSU KIFO CHA WAZIRI WA FEDHA TANZANIA DK WILLIAM MGIMWA

mgimwa 12Rais Jakaya Kikwete amepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa za kifo cha Waziri huyu wa fedha William Mgimwa na kwamba Taifa limempoteza katika kipindi ambacho linamuhitaji zaidi kutokana na mchango wake mkubwa.
 
Katibu mkuu kiongozi balozi Ombeni Sefue ambae ndio ametangaza kifo cha Waziri huyu kwa niaba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania, amesema Mgimwa amefariki saa tano na dakika 20 asubuhi hospitalini Afrika Kusini.
Maandalizi ya kuurudisha nyumbani mwili wa Marehemu yanafanywa na Serikali kwa kushirikiana na familia na kwamba taarifa zaidi zitazidi kutolewa kadri zitakavyopatikana.

Sunday, December 29, 2013

THEE BOSS LADY ''HUDDA MONROE AMPA DONGO JACKIE CLIFF KUHUSIANA NA SAKATA LA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA CHINA

Aliyekuwa muwakilishi wa Kenya kwenye shindano la Big Brother Africa ‘The Chase’,
Huddah Monroe aka Thee Boss Lady amerusha dongo kwa mrembo wa Tanzania Jackie Cliff ambaye alikamatwa na dawa za kulevya aina ya Heroin nchini china.

Tweet ya Huddah inadai kuwa Jackie Cliff ni mrembo ambaye alitaka kuishi maisha mazuri ya haraka na kutumia vitu vya kifahari, pia akaambatanisha na picha mbili zinazomuonesha Jackie akiwa amepozi kabla ya kukamatwa na nyingine akiwa na pingu, picha iliyotolewa na gazeti la nchini China.
View image on Twitter
Beautiful girl...Wanting to live the "Fast Life" "The good life" Gucci ,Prada,Roberto Cavalli,Alexander Wang!
Katika tweet nyingine Huddah ambaye hupenda kuonesha maisha ya kifahari anayoishi,  amefunguka zaidi na kuonesha kuwa yeye ni muoga na asingeweza kufikia kiwango hicho.
“So this beautiful Tanzanian girl was caught with a KG of Cocaine. 
 
That’s now a BAD ASS B**CH! I’m such a coward…I swear I’m not BAD!” Huddah ametweet.

PREZZO AMJIBU JAGUAR KWA KUONESHA GARI LAKE JIPYA LENYE THAMANI KUBWA.

Unaambiwa wiki moja baada ya staa wa muziki Kenya (Jaguar) kuonyesha gari lake jipya aina ya Jaguar ambalo alionekana nalo alipokwenda kufanya show, zimetoka picha za nje ndani za gari analotembelea rapper CMB Prezzo wa Kenya ambae mara kadhaa waliingia kwenye headlines na Jaguar kwa malumbano mbalimbali ikiwemo kutambiana muziki, mali na uwezo wa kifedha.
 
Gari la Jaguar lenye thamani ya shilingi Milioni 16 za Kenya ambalo liko mwisho wa hii post, aliiingia nalo kwenye uwanja pembeni kabisa ya jukwaa alipokwenda kufanya show ambapo alishuka kwenye gari wakati time yake ya kupanda jukwaani ilipofika, alikua kalipaki karibu kabisa na ngazi za kupandia jukwaani.

Hili ndio Gari ya Jaguar

MSANII DAYNA NYANGE AKANUSHA KUHUSIANA HABARI ZILIZO KUWA ZIMEENEA KUHUSIANA NA KUFANYA UCHAFU UFUKWENI

Mwana muziki wa Bongo freva toka mkoani    Morogoro mwana dada Dayna Nyange, amekanusha kuhusishwa na picha 

zilizomuonesha akifanya uchafu ufukweni akiwa na njemba nusu uchi.  Dayna kupitia page yake ya facebook, ameweka wazi kwamba sivyo kama ilivyoandikwa na baadhi ya mitandao kwamba alfumwa badala yake ilikuwa ni sehemu ya location ya video yake ya wimbo mpya wa mimi na wewe


"Jamani Hizi ni moja ya Picha.... Tulipokuwa location tuna shoot wimbo wangu wa "Mimi Na wewe" Na sivyo kama ilivyo semekana. Na baadhi ya blogs kwamba nimefumwa beach nikijiachia sijui nini Na nani kha!

Thursday, December 12, 2013

AUDIO & VIDEO | DAYNA NYANGE - MIMI NA WEWE


Labels