Pages

Sunday, January 05, 2014

BREAKING NEWS: BOTI YA MV KILIMANJARO II KUTOKA PEMBA KUELEKEA UNGUJA YANUSURIKA KUZAMA

Habari zilizotufikia hivi punde zinasema boti ya Kilimanjaro 2 iliyokuwa ikitoka Pemba kuelekea Ugunja inasemekana imepingwa na dhoruba kali na kunusurika kuzama, inadaiwa kuna vifo vimetokea. 
 
Ukweli ni kwamba wimbi kubwa liliipiga boat na kusababisha hali ya tafrani. Nimetoka kuongea na mamlaka ya bandari sasa hivi na boat iko njiani inakuja unguja iko maeneo ya Beit ras sasa hivi. Haijazama  na iliondoka na abiria watu wazima 269, watoto 60 na mabaharia 8 wote wako salama.

Wimbi kubwa liliipiga likachukua mabegi na baadhi ya life jackets. Injini za boat zilizima, ilibidi watulie kwa muda kuona kama wimbi lilichukua na baadhi ya abiria lakini hakuna hata mtu mmoja aliyeachwa.
 
Nakumbuka mamlaka ya hali ya hewa walitoa tahadhari kuhusu mchafuko wa bahari hizi siku.

CHANZO:-JAMII FORUM NA CLOUDS FM

0 maoni:

Post a Comment

Labels