Pages

Tuesday, November 12, 2013

SHIRIKA LA TUNAJALI (WE CARE) LINATARAJIA KUZINDUA MRADI WA ZERO VVU KWA MIKOA YA IRINGA NA NJOMBE

 
Picha na aminia website
 
Na Veronica Mtauka
 
Shirika la TUNAJALI linatarajia kuzindua mradi wa zero Vvu katika mkoa Njombe na Iringa ili kutokomeza maambukizi mpya ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Hayo yamebainika mapema hii leo mjini Makambako mkoani Njombe kwenye kikao cha wadau na wanahabari wa vyombo vya habari vya mkoa wa Njombe na Iringa ambapo wanahabari hao wametakiwa kuwa chachu ya kutumia vyombo vyao vya habari katika kutoa elimu kuhusu tiba ya ART kwa maisha yote kwa wajawazito na wanaonyonyesha wenye maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

Katika kikao hicho imebainika kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kupunguza viwango vya maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Tanzania imelenga kutokomeza maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi miongoni mwa watoto na kuwafanya akina mama waishi kwa muda mrefu zaidi.

Mpango huu umezinduliwa na mh. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania DR.Jakaya Mrisho Kikwete mkoani Lindi siku ya Ukimwi duniani mwaka 2012 na umeadhimia kufikia malengo ya kutokomeza maambukizi hayo kutoka asilimia 26 mwaka 2011 hadi asilimia 4 ifikapo mwaka2015.

0 maoni:

Post a Comment

Labels