Pages

Friday, December 06, 2013

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela amefariki dunia.

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela amefariki dunia. 
 
Mandela anaejulikana kama mpigania uhuru, usawa na haki za binadamu atakumbukwa kwa kujitoa kwake katika kuhakikisha watu weusi wanapata haki sawa katika ardhi yao toka kwa utawala wa makaburu kitu kilichofanya atumikie kifungo cha miaka 27 gerezani na hatimaye kuachiwa huru na kuwa rais wa kwanza mweusi nchini Afrika Kusini. 
 
Dunia nzima imepokea kwa mshituko taarifa za 
kifo cha Mandela huku Rais Jakaya Kikwette akiamuru siku 3 za maombolezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti. Pumzika kwa amani Tata Madiba.
 

0 maoni:

Post a Comment

Labels