Pages

Wednesday, September 25, 2013

RAPPER J COLE KUWARUDISHA TLC


Rapper J. Cole amesema anamategemeo makubwa kwenye mauzo ya album yake mpya ya Born Sinner na kuwa hivi karibuni mambo yakienda vizuri itafika mauzo ya Platinum yani kuuza copi milioni moja dunia nzima.

Rapper huyu anayesimamiwa na lebel ya Jay Z, Roc Nation amesema Tour yake ya 'What Dreams May Come' itafanikiwa kwasababu ya ubora wa album.

Kuhusu kufanya kazi na TLC, J Cole amesema tayari amesharekodi wimbo wake na kuwashirikisha TLC “Crooked Smile’ Nakuendelea kusema kuwa Chilli na T-Boz wamefanya kazi nzuri kwenye wimbo huo na atakuwa na mchango mkubwa kwenye kutengeneza album mpya ya TLC.
Fahamu kuwa mabinti hawa wamekuwa wakizungumzia cd yao mpya kwa muda mrefu sasa bila kutoa wimbo wowote redioni na sasa rapper J Cole ata hakikisha rekodi zao mpya zinakubalika.

0 maoni:

Post a Comment

Labels