Pages

Wednesday, September 25, 2013

VITUKO VYA WATOTO KWENYE MATAMASHA YA BURUDANI

 Aaaaah... Bro' unapeleka wapi huo mkono sasa ayiiiii... au ndiyo mnajipaga raha kiasi hiki mkija kwenye burudani zenu dah! kuanzia leo siachi kuzamia starehe za wakubwa, na siku nikikua nitafidia hivi ninavyovikosa leo, maana ukubwa kumbe rahaaa... mama yangu uuuwiiiiii...

Ama kweli si kila anayeenda kwenye starehe ya muziki hua analengo la kuangalia wasanii wanaofanya makamuzi kwa stejini, Nasema hivi baada ya kubaini picha hii hapo juu ambayo inamuonyesha kijana huyu aliyebahatika kuzamia kwenye tamasha la muziki  wa kizazi kipya na matokeo yake akashindwa kuangalia burudani iliyokuwa ikitolewa jukwaani na kuanza kucheki wakubwa zake waliokuwa wakikata ngoma kwa raha zao,angalia vizuri picha hii maana inafurahisha sana na dogo alianza kukodoa jicho katika picha ya chini ambayo inaonyesha hakulidhika sana na kujiweka vyema ili aone mkono wa jamaa ulikuwa ukipapasa sehemu gani ya mwili wa mrembo huyo.
Picha hii ukiangalia kwa makini utagundua kuna vijana watatu hapo akiwemo huyo hapo kulia ambaye ametumika kwenye picha ya juu,wao wamenifurahisha baada ya kuwaona kaka zao wakijipa raha na dada yao wakaachana na kuangalia shoo jukwaani badala yake wakageuzia macho upande wa pili tena wakionyesha hali ya kushangaa kinomanoma kama picha unavyoiona.

0 maoni:

Post a Comment

Labels