Pages

Monday, February 24, 2014

PROFESSOR JAY NA MRISHO MPOTO WAMEPATA SHAVU LA UBALOZI WA KAMPENI YA KILIMO

Professor Jay ameiambia Bongo5 kuwa wamesaini mkataba wa mfupi na tayari wameshaanza majukumu ya kazi ya kuhamasisha vijana kufanya kilimo mkoani Iringa.
 Mrisho Mpoto akiwa na Professor Jay Iringi
“Watu waliotuteua wanaitwa Ansaf lakini wawakilishi wa serikali ya United States of America ambayo inaitwa ‘One’ kwahiyo hapo kuna Ansaf na One ndio wanetuteua sisi kuwa mabalozi,” amesema Jay.

“Wamesema tuanze kuifanya kwasababu inatakiwa ifanyike kwa wakati huu na hatujasaini mkataba mrefu, tumesaini mkataba tu wa kuwaambia kazi zao walizotaka tufanye Iringa, tumeenda na kuzifanya kwa utiifu kabisa, kwa uaminifu kabisa na kwa uaminifu kabisa na tumewajulisha watu wetu waweze kufanya lakini wametuambia tunaweza kufanya vitu kwa mkataba muda mrefu kidogo.”

0 maoni:

Post a Comment

Labels