Pages

Wednesday, May 07, 2014

Nikki wa Pili: Weusi ni Kundi bora zaidi la hip hop Afrika Mashariki




Kundi la Weusi linaloundwa na Rappers watano kutoka Arusha [Nikki wa II,Joh Makini,G-Nako,Bonta Maarifa]lilitajwa kuwa kundi bora la muziki wa kizazi kipya katika KTMA 2014.

Msemaji wa kundi hilo Nikki wa Pili amesema kundi hilo sio tu ni kundi bora la hip hop Tanzania bali ni kundi bora la hip hop Afrika Mashariki.

Ameongeza kuwa kwao kupata au kutopata tuzo lengo lao ni kupiga hatua mbele kila mwaka na kuvuka mipaka ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.   

Wimbo wa Nikki wa Pili ‘Nje ya Box’ aliowashirikisha Joh Makini na G-Nako ulishinda tuzo ya wimbo bora wa hip hop katika KTMA2014.

Lakini pia kunamzigo mwengine mpya kutoka kwa Nikki wa II kutoka kwenye kundi la Weusi, na sasa anasema "Staki Kazi" ndani yake kuna vionjo vya RnB akiwa amemshirikisha Ben Pol pamoja na G-Nako huku ngoma ikiwa imetengenezwa na Nahreel wa Switch Records Joint hiyo itadrop town Tarehe 13.05.2014.

0 maoni:

Post a Comment

Labels