Pages

Monday, May 13, 2013

KOCHA MANCINI ATIMULIWA MAN CITY

Roberto Mancini alitwaa kibarua Man City Desemba 2009 alipotimuliwa Mark Hughes na kuiongoza kutwaa FA CUP Mwaka 2011 na Ubingwa wa England 2012 lakini mara baada ya Jumamosi kufungwa Fainali ya FA CUP Bao 1-0 na Wigan kipigo ambacho kinafuatia kupokonywa Ubingwa wao na Mahasimu wao Man United.
 http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02440/Roberto_Mancini_2440105b.jpg
Mara baada kufungwa na Wigan kwenye FA CUP, Mancini alikurupuka na kuulaumu uongozi wa Man City kwa kutokanusha uvumi wa Pellegrini, Raia wa Chile, kuja kutwaa kazi yake.
Hata hivyo, baadhi ya Wachambuzi huko England wamemponda Mancini na kudai hana haki ya kuilaumu Man City kwani hata yeye alipoteuliwa kwenda Klabu hiyo Mark Hughes alikuwa bado Meneja.
Ingawa Mancini aliiwekea Man City historia nzuri ya kutwaa Kombe lao la kwanza baada ya Miaka 35 walipotwaa FA CUP na kutwaa Ubingwa wao wa kwanza baada ya Miaka 44, kumaliza Msimu huu kwa ukame kunadaiwa kuwakera Wamiliki Matajiri wa Man City toka Falme za Nchi za Kiarabu ambao Jumamosi walikuwa Wembley kushuhudia Timu yao ikitwaa Kombe kwa mgongo wa ‘vibonde’ Wigan lakini wakajikuta chali baada ya kutunguliwa Bao 1-0 na Kombe la FA CUP kwenda Wigan, Timu ambayo huenda Msimu huu ikaandika Historia ya kuwa Klabu ya kwanza kutwaa FA CUP na kushushwa toka Ligi Kuu Msimu huo huo.


0 maoni:

Post a Comment

Labels