Pages

Thursday, April 18, 2013

LINEX The V.O.A KUFANYA NGOMA NA WYREE

Msanii Linex jana amekamilisha ndoto yake ya siku nyingi kufanya kazi na msanii maarufu kutoka Kenya "Wyre", ngoma hiyo ambayo kwa msaada wa digitali inaelekea kukamilika, imetengenezwa beat na producer Fundi Samweli ambae yupo Sweden kwa hivi sasa, ambayo ilitumwa kwa Linex na kuipeleka kwa producer Mswaki ambae pia ameongezea maujuzi yake, na hapo ndipo linex akaingiza sauti zake.

Hatimae leo beat na vocal za Linex zimetumwa Kenya kwa ajili ya Wyre kuingiza sauti leo usiku na kisha kuongezea maujuzi pia akiwa kama producer..kuonyesha furaha ya kukamilisha asilimia kubwa ya kazi hiyo Linex ameamua kushare na mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa facebook kwa kuandika status hii

Linex Sunday
Siku ya leo imekua nzuri sana kwangu nimepiga kazi na mtu nnaemzimiaga kitambo linex ft wyre cumn soon but sita ahidi ni lini itatoka but saiz ndo kazi imeisha God is good

0 maoni:

Post a Comment

Labels