Pages

Wednesday, April 17, 2013

PIGO LINGINE! Bi Kidude amefariki dunia mapema leo mjini Zanzibar

 
Mwimbaji maarufu wa muziki wa Taarabu Fatuma binti Baraka maarufu kama Bi. Kidude amefariki dunia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu, tangu mwaka jana. 

Taarifa hii imepatikana hivi karibuni kutoka katika vyombo mbalimbali vya habari, ambavyo baadhi yake vimedai kuthibitisha kifo cha gwiji huyo wa muziki, ambaye ni maarufu ndani na nje ya Tanzania. 

PIGO LINGINE! Bi Kidude amefariki dunia mapema leo mjini Zanzibar. mara kadhaa Bi kidude, ambaye amejipatia sifa na umaarufu ndani na nje ya nchi, amekuwa akizushiwa kifo kutokana na kuuguawa muda mrefu....taarifa zaidi za kifo chake endelea kufuatilia mtanda wako wa GPL...MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI--AMIN!
AMESHAZUSHIWA KIFO MARA KADHAA...TUJIKUMBUSHE MATUKIO YA NYUMA:
 
 
Usiku wa kuamkia leo ujumbe ulisambazwa kwenye mitandao ya simu za mkononi na mitandao ya kijamii, Facebook na Twitter kuwa Bi Kidude amefariki dunia! Moja ya SMS hiyo ilisomeka: Qaallu Inna Lillahi Wainna Ilaihi Raajiuni; BI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA! Habari ambazo zimekanushwa vikali na mwenyewe leo asubuhi. Kudhidirisha kweli hajafa, Bi. Kidude aliongea moja kwa moja na Radio One na kumwambia mtangazaji aliyetaka kujua ukweli wa habari hizo kwa kumjibu: "Maiti haiongei, mimi ndiye Bi Kidude, mzimaaa!" HII NI TABIA AMBAYO INAKUWA KWA KAZI YA KUZUSHIA WATU VIFO KWA KUTUMIA MITANDAO YA SIMU NA KIJAMII

0 maoni:

Post a Comment

Labels