Pages

Monday, September 17, 2012

Nas na Kelis warudiana?




Nas na Kelis wanaweza kuwa waliachana kwa talaka mbaya miaka mitatu iliyopita lakini inaonekana kama siku za uaudui zimekwisha.

Wawili hao walionekana kwenye chakula cha usiku pamoja wiki iliyopita na sasa wameonekana wakiwa pamoja na mtoto wao wa kiume Knight huko Santa Barbara.

Picha hizo zilichukuliwa na wapiga picha wa TMZ.
Nas na Kelis wakiwa na mtoto wao Knight

Hata hivyo wanandoa hao wa zamani wamekuwa wakisisitiza kuwa wao ni marafiki tu na wameamua kupatana kwa manufaa ya Knight.
Pia albam ya Nas, Life Is Good inazungumzia uhusiano na ndoa yake na Kelis ambayo huenda imefanya wawe karibu tena.

0 maoni:

Post a Comment

Labels