Pages

Monday, September 24, 2012

MSECHU KUREKODI NYIMBO NA VIDEO MPYA MAREKANI



Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Peter Msechu amesema anatarajia kufanya nyimbo na video nchini Marekani.
 
msanii huyo anasema kuwa ataenda nchini Marekani hivi karibuni na hajajua atarudi lini maana atafanya shoo mbalimbali

Msechu alisema hajajua ni nyimbo gani atazifanya akiwa huko ila amepania kufanya mazuri katika shoo zitakazofanyika mjini Washinton Dc, Houston Texas, Chicago, na New York. 
 
“Nimekuja huku kikazi zaidi kufanya shoo na kuandaa nyimbo zangu mpya na video zake” alisema Msechu

“Sijui nitakaa huku kwa muda gani mwaka huu unaweza kuisha au miaka kadhaa yote ni kuandaa mambo mazuri kwa mashabiki zangu” alisema

0 maoni:

Post a Comment

Labels