Pages

Wednesday, March 20, 2013

KILIMANJARO MUSIC AWARDS 2013 YAZINDULIWA LEO RASMI JIJINI DAR ES SALAAM

Meneja wa Kinywaji cha Kilimanjaro, George Kavishe akizungumza leo

Tuzo za muziki maarufu kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2013 zimezinduliwa leo jijini Dar es Salaam zikiwa na dhumuni kubwa la kutambua wasaniii waliopata mafanikio katika sekta ya muziki kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita, sambamba na kuasiniwa kawa mkataba wa udhamini wa Tuzo hizo kati ya kampuni ya TBL na BASATA kwa miaka mingine mitano.

 

Meneja wa  kinywaji cha Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe amesema kuwa, “Kilimanjaro Premium Lager inajivunia kuendelea kudhamini  tuzo hizi kwa mara ya 12 sasa lengo likiwa kukuza muziki nchini Tanzania. Mchakato wa kuwapata wanamuziki bora wa mwaka unaanza leo na utamalizika tarehe 8 Juni ambapo tutakuwa na hafla ya usiku maalum wa kwa ajili ya kutangaza washindi.”
Hapa pia ni tukio la kuzinduliwa rasmi kwa nembo  ya Kilimanjaro Music Award 2013 (Katika picha wa kwanza kulia ni Kushilla Thomas Mkurugenzi wa Masoko wa TBL na Godfrey Mngereza Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA kushoto pamoja na Maofisa wa TBL na BASATA).
Nembo Mpya
George amesema Kilimanjaro Premium  Lager imejizatiti kuendeleza tasnia ya muziki Tanzania kwa kutambua na kuwapa tuzo wasanii wenye vipaji, lengo lao kubwa likiwa ni kuongezea thamani kazi na wasanii wa hapa hapa nyumbani na pia kuwafungua macho watanzania kuzidi kuona thamani ya muziki wa nyumbani pia kutambua mchango wa wanamuziki katika kuleta maendeleo ya nchi.

Kusainiwa kwa mkataba mpya na BASATA ni uthibitisho wa azma kubwa tuliyonayo katika kuendeleza muziki wa Tanzania, dhamana ambayo sasa wanaishikilia kupitia tuzo hizi mpaka mwaka 2018.
Alikuwepo pia Chidi Benz Chuma kuwakilisha wasanii wa muziki Tanzania ambapo alizungumzia matarajio yake makubwa katika maboresho ya tuzo za mwaka huu.
Some of the pictures courtesy of John Bukuku

0 maoni:

Post a Comment

Labels