Pages

Sunday, March 10, 2013

Mabingwa watetezi, Simba wamefufuka katika jinamizi la matokeo mabovu baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Wagosi Coast Union.

SIMBA 2-1 Coastal Union

Mabingwa watetezi, Simba wamefufuka katika jinamizi la matokeo mabovu baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Wagosi Coast Union. Simba ambao walianzisha wachezaji wengi wa kikosi cha vijana walionekana kuwa na uchu wa mabao toka dakika ya mwanzo huku Mrisho Ngassa akionekana kuwa mwiba mkali kwa walinzi wa Coastal Union, na ilikuwa ni katika dakika ya 45 alipoipatia bao la kwanza. Wakati bado Coastal wakitafakari nini kimetokea, Haruna Chanongo alifunga bao la pili baada ya kugongeana vizuri na Ngassa na hadi mapumziko Simba walikuwa wakiongoza. Kipindi cha pili Coastal walipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Razack Halfan huku Simba wakiendelea kumiliki mpira kwa asilimia kubwa. Hadi mwisho Simba 2-1 Coastal Union.
Mabingwa watetezi, Simba wamefufuka katika jinamizi la matokeo mabovu baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Wagosi Coast Union.
Simba ambao walianzisha wachezaji wengi wa kikosi cha vijana walionekana kuwa na uchu wa mabao toka dakika ya mwanzo huku Mrisho Ngassa akionekana kuwa mwiba mkali kwa walinzi wa Coastal Union, na ilikuwa ni katika dakika ya 45 alipoipatia bao la kwanza. 
Wakati bado Coastal wakitafakari nini kimetokea, Haruna Chanongo alifunga bao la pili baada ya kugongeana vizuri na Ngassa na hadi mapumziko Simba walikuwa wakiongoza.
Kipindi cha pili Coastal walipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Razack Halfan huku Simba wakiendelea kumiliki mpira kwa asilimia kubwa. Hadi mwisho Simba 2-1 Coastal Union.

0 maoni:

Post a Comment

Labels