Pages

Tuesday, August 06, 2013

FAHAMU ZAIDI MPANGO WA HEMEDY PHD NA MR BLUE HAPA

Baada ya kuwa na maswali mengi kwa Hemed PhD kuhusiana na kuchelewa kwa video ya ngoma yake ambayo amefanya na Mr Blue 'Rest of my Life', msanii huyu ameweka wazi kuwa mnchongo wa kupiga picha za video hii utaanza rasmi baada ya kukamilika kwa mwezi wa Ramadhani.
Hemed amesema kuwa, Video hii imeshindwa kufanyika kwa muda sasa kutokana na Mr Blue kuwa na mishe mishe mbalimbali ikiwepo safari za nje.
Hemed ameweka wazi kuwa, Mwishoni mwa mwezi huu tarehe 30 itakuwa anasherekea siku yake ya kuzaliwa, siku ambayo pia amepanga kufanya kuzindua video hii ambapo mipango inaonyesha kuwa utakuwa imekwishakamilika na itakuwa ni bonge la 'kioo' a.k.a Video.

0 maoni:

Post a Comment

Labels