Pages

Sunday, December 16, 2012

ALBUM MPYA YA RAPPER THE GAME "JESUS PIECE" YASHUTUMIWA KUDHALILISHA UKRISTO


game-jesus-piece-album-cover
Albam ya tano ya rapper wa West Coast Jayceon Taylor aka The Game iitwayo ‘Jesus Piece’ imeingia sokoni wiki hii na kusababisha hasira kubwa miongoni mwa waumini wa dini ya kikristu kutokana na kutumia alama zinazoikosea heshima dini hiyo.

Kava la albam hiyo lina picha ya Yesu mweusi akiwa amejifunika usoni bandana nyekundu na cheni yenye sura ya Yesu miongoni mwa alama zingine.

Mratibu wa mawasiliano wa shirika la Save Africa’s Children Tilla Amin Tanyi ameiambia website ya FoxNews kuwa The Game amemuonesha Yesu kama mtu wa kawaida anayetafuta mali za dunia na kushiriki kwenye vitendo vya kihalifu.

Albam hiyo ina nyimbo kadhaa zenye mashairi ya dini zikiwemo Heaven’s Arm na Pray.

Mwezi October mwaka huu alipolitambulisha kava la albam yake kwenye mtandao wa Instagram inadaiwa kuwa uongozi wa kanisa katoliki uliipigia simu label yake ya Interscope kutoa malalamiko yake.

Hata hivyo The Game anasema ameiitwa albam yake Jesus Piece kwasababu mwezi August alibatizwa na amekuwa akienda kanisani lakini hajaacha maisha yake ya kwenda club, kuvuta na kunywa

0 maoni:

Post a Comment

Labels