Pages

Saturday, December 22, 2012

KOIKOI NI UJIO MPYA WA MSANII OMMY DIMPOZ

   

Msanii anaefanya vizuri na kazi zake kama "Me & Una zingine si mwingine ni Ommy Dimpoz akaribia kuachia ngoma yake nyingine kwa fans na inawezekana ikawa funga mwaka 2012.
       
Ommy ambae kwa sasa anatamba na wimbo wake wa 'Me N You' ambao amemshirikisha Vanessa Mdee a.k.a V hivi amesema yupo karibu kuachia kamba hiyo inayokwenda kwa jina la Koikoi

Hivyo kama we ni shabiki mkubwa wa Ommy Dimpoz basi kaa tayari kwa kuisubiria ngoma yake hiyo inayofuata na kama kawaida jamaa huwa hakosei katika kazi zake.
     
Ommy Dimpoz ni msanii mwenye chimbuko la Kigoma aliyeanza kuvuma kwa kasi alipo-release ngoma yake ya kwanza inayofahamika kama Nai Nai ikimshirikisha AliKiba na baada ya hapo akaachia Baadae  ambayo pia ilifanya na inafanya vyema redioni na kwenye TV

0 maoni:

Post a Comment

Labels